photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> > WATOTO WA VIGOGO TANROADS WAFUKUZWA KWA KUGHUSHI

WATOTO WA VIGOGO TANROADS WAFUKUZWA KWA KUGHUSHI

Posted on Oct 25, 2012 | No Comments

SERIKALI imewafukuza kazi watoto wa vigogo waliopata ajira bila ya kufuata taratibu za kisheria katika mizani inayosimamiwa na Wakala wa Ujenzi wa Barabara(Tanroads).

Hata hiyo imekuja siku chache baada ya Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli kudai kuwa, kuna baadhi ya watoto wa vigogo wamepata ajira kinyume na taratibu.

Akizungumza katika kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuu (PAC), Mkurugenzi Mkuu wa Tanroads, Mhandisi Patrick Mfugale  alisema watoto hao waliajiriwa kimakosa.
Alisema watoto hao wametambuliwa na kwamba baadhi yao tayari wamechukuliwa hatua za kinidhamu ikiwa ni pamoja na kufukuzwa kazi huku wengine vyeti vyao vikiendelea kukaguliwa.

“Kuna baadhi ya wafanyakazi walikuwa wamepata ajira kinyume na taratibu, hii inatokana na kupata ajira kwa kujuana lakini suala hili tayari tumelifanyia kazi na baadhi yao tumewafukuza,” alisema Mhandisi Mfugale.

Alisema kutokana na hali hiyo, wataendelea kuhakiki vyeti vya wafanyakazi wote na kuhakikisha kuwa, wanatangaza ajira upya ili wenye vigezo waweze kupitishwa na wasiokuwa navyo waondolewe.

Alisema mkakati uliopo ni kuhakikisha kuwa, ajira zinazotolewa katika idara hiyo ni za muda mfupi, ili kuondoa mianya ya ajira za kujuana.

Aliwataka  mameneja wote wa mikoa kufuata taratibu za kisheria  katika kutoa ajira kwa wafanyakazi wapya.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru