photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> RAIS ASSAD APEWA SAA 48 KUONDOKA NCHINI SYRIA.

RAIS ASSAD APEWA SAA 48 KUONDOKA NCHINI SYRIA.

Posted on May 31, 2012 | No Comments

Waasi wa Syria wamempa Rais Assad muda wa  saa 48 wa kutekeleza mpango wa amani wa  kimataifa ili kukomesha mauaji la siyvo ataona matokeo yake.
Katika tamko alilolitoa kwenye mtandao wa “You  Tube”, Kanali Qassim Saadeddine amesema waasi watajitoa katika mapatano yote, hadi itakapofika leo adhuhuri na kuchukua hatua za kuwalinda raia na vijiji vyao.
Wakati huo huo Urusi na China zimeusisitiza msimamo wao wa kupinga kujiingiza kijeshi nchini Syria.
Hapo awali mjumbe wa kimataifa anaesuluhisha nchini Syria Bw. Kofi Annan amesema kuwa nchi hiyo  sasa imefikia hatua ambapo hali inaweza kuwa  mbaya zaidi.
Wakati mapigano yanaendelea kati ya waasi na majeshi ya serikali, waangalizi wa kimataifa  walizigundua maiti 13 mashariki mwa Syria.
Miili yao ilikuwa imefungwa na kuonyesha dalili kwamba waliuliwa kwa kupigwa risasi.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru