photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> ASHA ROSE MIGIRO AANGWA RASMI UN.

ASHA ROSE MIGIRO AANGWA RASMI UN.

Posted on Jun 30, 2012 | No Comments

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa akiwa na Mkewe, anayefuatia ni Naibu Katibu Mkuu, Dkt. Asha-Rose Migiro akiwa na Mumewe,  Profesa Cleophas Migiro wakisubiri kusalimiana na wageni waalikwa wakati wa hafla ambayo Ban Ki  Moon aliandaa maalum kwajili ya kumuaga msaidizi wake wa Karibu.
Profesa Migiro akiwa na Bint yake, Chansa- Jasmin wakifuatilia hafla hiyo kwa makini.
Ban Ki Moon akizungumza wakati wa hafla hiyo ambapo amempogeza na kushukurusu sana Migiro kwa namna alivyokuwa mshauri wake na mwalimu wake ambaye a anasema kwa  ualimu wake anampa alama ya plus plus plus. akatumia hafla hiyo kutangaza kwamba anamteua   Dkt. Asha- Rose Migiro kuwa mjumbe wake maalum katika  masuala ya ukimwi na ugonjwa wa ukimwi   Barani  Afrika. Migiro anaondoka  baada ya kuutumikia Umoja wa  Mataifa kwa miaka mitano na nusu.
Dkt. Asha-Rose Migiro akizungumza wakati wa hafla hiyo, akatoa shukrani zake kwa  Ban ki Moon kwa kumpatia heshima hiyo ya kihistoria ambayo haita kaa ifutike na kwamba  ameupokea uteuzi huo kwa mikoni miwili na hasa kutokana na kwamba tatizo la ugonjwa wa ukimwi ni tatizo ambalo analichukulia kwa uzito wa aina yake.

Hata kupiga picha naweza. Naibu Katibu Mkuu akinyaka  tukio hili la picha wakati Katibu Mkuu Ban Ki Moon akizungumza na Bint wa mwisho wa Migiro Chansa Jasmin.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru