photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> > WANAFUNZI WATANO WAFARIKI NCHINI UGANDA BAADA YA MABWENI KUUNGUA MOTO.

WANAFUNZI WATANO WAFARIKI NCHINI UGANDA BAADA YA MABWENI KUUNGUA MOTO.

Posted on Jun 27, 2012 | No Comments

Wanafunzi watano wameteketea kwa kuungua kwa moto nchini Uganda baada ya moto kuunguza mabweni mawili ya Leos Junior Academy katika manispaa ya Masaka.
Wanafunzi wote waliofariki ni wa elimu ya msingi ambao wameungua hadi kutotambulika, na miili yao imepelekwa katika hospitali ya rufaa ya Masaka.
Kamanda wa Polisi wa Kanda ya Kusini Simon Peter Wafana amesema tayari polisi nchini humo imeanzisha uchunguzi wa chanzo cha moto huo.
Hii ni mara ya pili moto kuzuka katika shule hiyo katika kipindi cha miaka miwili.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru