Wanawake kijiji cha ifigo mbeya wadai maji machafu wanayotumia yanawasababishia ugonjwa wa kichocho..
Posted on
Jun 12, 2012
|
No Comments
Na Francis Godwin Blog,Mbeya
WANAWAKE wa kijiji cha Ifiga kata ya Ijombe wilaya ya Mbeya mkoani Mbeya wamedai kuwa tatizo la maji katika kijiji hicho limeendelea kuwa sugu na kupelekea kutumia maji ya kisima ambayo si safi na salama na kujikuta wakiendelea kukumbwa na tatizo la ugonjwa wa kichocho .
Wakizungumza na timu ya wanahabari wanaharakati wa mtandao wa jinsia Tanzania (TGNP) waliotembelea kijijini hapo leo wanawake hao walisema kuwa kijiji hicho kutokana na ukosefu wa huduma hiyo ya maji wamekuwa wakilazimika kuchota maji katika kisima kimoja kilichoppo kijijini hapo ambacho maji yake si lazima kwa afya za binadamu.
Alisema Sophia John kuwa kisima hicho kimekuwa kikitumia na wakazi zaidi ya 2000 wa kijiji hicho na kuwa pamoja na kuwa maji hayo si salama baadhi ya watu hasa watoto wamekuwa wakiyanywa pasipo kuchemcha hali inayochangia kuongezeka kwa idadi ya wagonjwa wa kichocho katika kijiji hicho.
John alisema kuwa mbali ya watoto wa kijiji hicho kukumbwa na tatizo la ugonjwa wa kichocho kutokana na huduma hiyo ya maji wanayoitumia kuwa si salama bado wamekuwa wakichangia mradi wakiiomba serikali kusaidia kutatua tatizo hilo bila mafanikio .
Kwani alisema wanananchi wa eneo hilo hasa wanawake na watoto wamekuwa wakiathirika zaidi na tatizo la ukosefu wa maji kutokana na kisima hicho kuwa mbali na makazi yao hivyo wakati mwingine kutumia muda wa masaa manee hadi 6 kwenda kufuata huduma hiyo ya maji Kisimani .
