photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> > JE, WAJUA TAKRIBANI WANAUME 15000 DAR ES SALAAM HULALA NA MACHANGUDOA KILA SIKU.

JE, WAJUA TAKRIBANI WANAUME 15000 DAR ES SALAAM HULALA NA MACHANGUDOA KILA SIKU.

Posted on Oct 21, 2012 | No Comments

Shocking: Wanaume 15,000 Dar es Salaam hulala na machangudoa kila siku Kwa mujibu wa utafiti wa Mpango wa taifa wa kudhibiti ukimwi nchini –NACP, kwa kushirikiana na Wizara ya afya na ustawi wa jamii jumla ya wanaume 15,000 wateja wa wanawake wanaojiuza (machangudoa) nchini.
Utafiti huo mpya uliofanyika kwenye wilaya tatu za Dar e Salaam, Temeke, Ilala na Kinondoni umebaini kuwa  wanawake wanaofanya biashara ya ngono  wanafikia 7,500 huku kila mmoja akiwa na wateja watatu kwa siku.
Sababu ya kufanyika utafiti jijini Dar es Salaam ni kutokana na Idadi kubwa ya watu na muingiliano wa tamaduni katika maeneo kadhaa zikiwemo klabu za usiku, mahotelI na maeneo mengine yasiyo rasmi ambapo biashara ya ngono hufanyika kwa kiasi kikubwa na kuashiria ongezeko maambukizi ya ukimwi.
Pia matokeo ya ufuatiliaji wa wanawake wanaojiuza Dar es salaam pekee  umebaini kuwa kiwango cha maambukizi ni asilimia 31.4 ukilinganisaha na asilimia 10.4 ya kiwango cha maambukizi kwa wanawake wote jijini Dar es Salaam, lakini je hali hii ipoje kwa mikoa mingine?

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru