photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> > KAMISHNA WA UMOJA WA ULAYA AAMUA KUACHIA WADHFA WAKE BAADA YA KUKUMBWA NA KASHFA.

KAMISHNA WA UMOJA WA ULAYA AAMUA KUACHIA WADHFA WAKE BAADA YA KUKUMBWA NA KASHFA.

Posted on Oct 17, 2012 | No Comments

 
Kamishna wa Umoja wa Ulaya anayehusika na masuala ya Afya amejiuzulu kutokana na kashfa za rushwa.
Kamishna huyo John Dalli kutoka Malta amechukua uamuzi wa kuachia madaraka hayo baada ya kitengo cha Umoja wa Ulaya cha kupambana na ufisadi kugundua kwamba mjasliamali kutoka Malta alitaka kutumia ushawishi alio nao kwa kamishna huyo, kujipatia malipo kutoka kampuni ya sigara ya Sweden.
Mjasliamali huyo amedai kwamba angeweza kusimamisha sheria ya Umoja wa Ulaya inayohusu matumizi ya tumbaku.
Halmashauri ya Ulaya ilisema haina ushahidi kwamba Dalli alihusika moja kwa moja katika kashfa hiyo, lakini imesema inaamini kwamba alifahamu kilichokuwa kikiendelea.-DW.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru