MTETEZI WA WANAWAKE ANUSURIKA KIFO DRC
                              Posted on 
                              Oct 26, 2012
                            |
                            
                                  No Comments
                                  

Wanawake waathirika wa ubakaji 
Mtetezi maarufu wa wathiriwa wengi wa ubakaji katika Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo amenusurika jaribio la kumuua.
Daktari Denis Mukwege alishambuliwa na watu 
waliokuwa na bunduki nyumbani kwake Bukavu aliko na hospitali 
inayowahudumia waathiriwa wa dhulma za kimapenzi.
Alihepa risasi lakini mlinzi wake aliuawa katika tukio hilo.
Daktari Mukwege ni mpasuaji mashuhuri duniani na
 ameshinda tuzo nyingi tu kimataifa kwa juhudi zake kutetea wanawake 
wanaobakwa na makundi ya waasi.
 
 
 
 
 
 
 
 
