photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> > TANZANIA YAIAMBIA MALAWI, FANYA UTAFITI WA MAFUTA LAKINI MARUFUKU UPANDE WA ZIWA WA TANZANIA

TANZANIA YAIAMBIA MALAWI, FANYA UTAFITI WA MAFUTA LAKINI MARUFUKU UPANDE WA ZIWA WA TANZANIA

Posted on Oct 21, 2012 | No Comments

Tanzania imesema Malawi inaweza kuendelea na utafiti wa mafuta katika kaskazini magharibi ya Ziwa Nyasa, lakini marufuku kufanya utafiti huo nusu ya upande wa kaskazini mashariki sababu huo ni eneo la Tanzania.
Waziri mkuu wa Tanzania Mizengo Pinda aliiambia BBC, Alhamisi kwamba kwa mujibu wa sheria za kimataifa, Tanzania inamiliki nusu ya ziwa, hivyo Malawi inaweza kuendelea kufanya utafiti al muradi utafiti huo ufanyike upande wao na wasivuke mpaka, ambao ni katikati ya ziwa.
“Kama Malawi wanafanya utafiti, wafanye wakielewa kwamba kuna mpaka, na hakutakua na tatizo. Lakini wanafikiria kupuuza mpaka, kauli yetu kwao ni hapana, ziwa lote sio lenu” alisema PM Pinda.
Akijibu swali kwa nini askari wa Tanzania wanawasumbua wavuvi wa Malawi ziwani, PM Pinda alisema kama wavuvi hao wa Malawi wamevuka mpaka wa kimataifa, ambao ni katikati ya ziwa, askari wa Tanzania wana wajibu wa kuwakamata na kuwahoji.
“Ni kweli tuliwahoji kwanini wameingia katika eneo la Tanzania, tukawaambia warudi katika upande wao wa ziwa” alisema.
Aliongeza kwamba Tanzania inataka kumaliza mgogoro wa mpaka kwa amani. Na kwamba inataka amani ya muda mrefu kati ya nchi hizi mbili iendelee.
lake malawi ziwa nyasa tanzania Tanzania yaiambia Malawi, fanya utafiti wa mafuta lakini marufuku upande wa ziwa wa Tanzania

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru