photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> > TANESCO YAKATA RUFAA DHIDI YA HUKUMU YA KUILIPA DOWANS.

TANESCO YAKATA RUFAA DHIDI YA HUKUMU YA KUILIPA DOWANS.

Posted on Nov 20, 2012 | No Comments

 Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limekata rufaa katika Mahakama ya Rufaa Tanzania kuomba zuio la utekelezaji wa hukumu ya Mahakama Kuu, inayolitaka kuilipa Shilingi bilioni 96 Kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans.
Tanesco wamekataka rufaa hiyo ili kusitisha utekelezaji wa hukumu ya Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara (ICC), kama ilivyoamuliwa na Mahakama Kuu, iliyolitaka shirika hilo liilipe Dowans fedha hizo, ikiwa ni fidia ya kuvunja mkataba wa biashara kinyume cha sheria.
Rufaa hiyo iliwasilishwa Septemba 19 na imepangwa kusikilizwa Desemba 5 mbele ya jopo la majaji watatu.
Katika rufaa hiyo, Tanesco inaomba kusitishwa kwa utekelezaji wa uamuzi huo hadi kesi ya msingi inayoendelea katika Mahakama ya Kimataifa Divisheni ya Biashara itakapokwisha.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru