UGANDA KUPITISHA SHERIA MPYA YA USHOGA IKIWA NI ZAWADI YA CHRISTMAS KWA WANANCHI WAKE.
Posted on
Nov 16, 2012
|
No Comments

Uganda
inatarajia kupitisha sheria mpya dhidi ya ushoga kufikia mwishoni mwa
mwaka huu, ikiwa kama zawadi ya ‘Christmas, kwa wahusika wa mahusiano ya
jinsia moja.
Shirika
la Habari la AP limemkariri Spika wa Bunge la nchi hiyo Rebecca Kadaga
(pichani) akisema wananchi wanahitaji sheria hiyo.
Vitendo
vya kishoga ni marufuku na ni kinyume na sheria nchini Uganda na mswada
wa suala hilo uliowasilishwa bungeni unapendekeza adhabu kali kwa watu
watakaobainika.
Hata hivyo Wahisani wa nje wamekuwa wakitishia kusitisha misaada iwapo haki za mashoga nchini humo hazitatambuliwa.