photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> > MESSI KUTWAA TUZO YA MCHEZAJI BORA WA DUNIA KWA MARA YA 4??..

MESSI KUTWAA TUZO YA MCHEZAJI BORA WA DUNIA KWA MARA YA 4??..

Posted on Dec 3, 2012 | No Comments

 Christiano Ronaldo, Lionel Messi na Andres Iniesta wote wameorodheshwa kuwania tuzo ya  mchezaji bora wa mwaka huu ya Ballon d’Or.
Messi mshambuliaji wa Barcelona mwenye umri wa miaka 25, tayari ameshinda mataji hayo mara tatu na bado anapigiwa debe kushinda tena tuzo hii ambayo itatangazwa mjini Zurich mnamo Januari saba baada ya kura kupigwa na waandishi habari, manahodha wa timu za taifa pamoja na makocha.
Kama atashinda, anaweza kuwa mchezaji wa kwanza kushinda taji hilo mara nne, baada ya kujiunga na gwiji wa Ufaransa na rais wa sasa wa Shirikisho la Soka Ulaya UEFA Michel Platini kama wachezaji pekee kushinda mara tatu mfululizo. Nyota wa Uholanzi Johan Cruyff na Marco Van Basten pia wamewahi kushinda matatu.
 Mkufunzi wa Uhispania Vicente del Bosque ambaye aliongoza timu yake kushinda taji la UEFA EURO 2012 na kuwa wa kwanza kushinda vinyang’anyiro vitatu mfululizo ni miongoni mwa wanaopigiwa upatu kutwaa tuzo ya kocha bora na atapambana na Jose Mourinho wa Real Madrid na Pep Guardiola aliyekuwa wa Barcelona.
 Kwa upande wa tuzo ya mchezaji bora kwa wanawake, bingwa mara tano wa Brazil Marta atapambana na Wamarekani Aby Wambach na Alex Morgan.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru