ONYESHO LA TANO LA MWAKA LA TANZANIA RED RIBBON FASHION GALA 2012 LAKUSANYA SHILINGI MILIONI 72.
Posted on
Dec 2, 2012
|
No Comments

Mc’s
wa Onyesho la Mavazi la Red Ribbon Fashion Gala 2012 Abby Plaatjes na
Evance Bukuku wakikaribisha wageni na kutoa utaratibu wa shughuli nzima
katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

Mwanamitindo
wa Kimataifa nchini na Balozi wa Tanzania Mitindo House (TMH) Flaviana
Matata akifungua maonyesho hayo na vazi la Ubunifu wa Khadija
Mwanamboka.

Pichani
Juu na Chini ni Models wakionyesha mavazi mbalimbali yaliyobuniwa
kutokana na Vitenge vilivyotengenezwa na Kiwanda cha Vitenge cha
Morogoro Polytex ambacho ni moja wapo ya Makampuni ya MeTL.








Msanii
wa muziki wa Kizazi kipya Linex akiimba wimbo maalum wa kuhamasisha
jamii kusaidia watoto yatima na wanaoishi kwenye mazingira magumu kwenye
onyesho la Tanzania Red Ribbon Fashion Gala 2012.

Muasisi na Mwenyekiti wa Tanzania Mitindo House Bi. Khadija Mwanamboka (kulia) akimkabidhi cheti ushiriki kwa Meneja Masoko wa CFAO MOTORS Tharaia Ahmed (katikati).

Mwakilishi wa Kiwanda cha 21 CENTURY TEXTILE kinachotengeneza vitenge
vya Morogoro Polytex kilicho chini ya Kampuni za Mohammed Enterprises
Tanzania Ltd. (MeTL) Bw. Cosmas Mtesigwa akipokea cheti cha ushiriki
kutoka kwa Bi. Khadija Mwanamboka.
Morogoro Polytex ni kiwanda cha kuzalisha vitenge na chenye uwezo wa kuzalisha mita milioni 100 kwa mwaka na ndicho kiwanda kikubwa kwa sasa katika ukanda wa eneo la Afrika Mashariki.

Mwenyekiti wa Flaviana Matata Foundation Bi. Flaviana Matata akipokea cheti cha heshima kwa kushiriki kwenye onyesho la Tanzania Red Ribbon Fashion Gala 2012 ambalo limefanikiwa kukusanya kiasi cha Shilingi Milioni 72 kwa ajili ya kuwasaidia na kuwaendeleza watoto yatima wa kituo cha TMH wakiemo wenye kuishi na virusi vya Ukimwi.

Omari Salisbury wa Qway International wanaosambaza vinywaji vya Belvedere Vodka akikabidhiwa cheti kwa mchango wao kutambuliwa na TMH.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mabibo Beer Wines & Spirits Ltd –
Benedicta Rugemalira akitabasamu baada ya kupokea cheti kutokana na
kampuni yake kutoa mchango mkubwa katika kuwezesha ufanisi wa shughuli
ya kuchangisha fedha kwa ajili
ya kusaidia kituo cha watoto yatima cha TMH ambapo kampuni yake Mabibo
Beer Wines & Spirits ilihusika kikamilifu kunywesha wageni.

Wanamitindo Flaviana Matata na Jennifer Bash wakipita jukwaani na magauni yaliyotengenezwa na mbunifu wa kimataifa Sherri Hill wakiyanadi kwa wageni kwa ajili ya kuchangisha fedha za kusaidia kituo cha watoto yatima cha TMH.

MC Evance Bukuku akinadi gauni lililovaliwa na Mwanamitindo Jennifer Bash lililobuniwa na Sherri Hill.

Wanamitindo wakionyesha magauni hayo meza kuu ya wageni waalikwa akiwemo Mh. Zitto Kabwe.

Wageni waalikwa waliotia fora katika maonyesho hayo ambao walinunua magauni ya Sherri Hill kwa shilingi
Milioni 4.8 Anitha (Kushoto) na Milioni 4 Alma ( wa pili kushoto) ikiwa
ni mchango wao katika onyesho la Tanzania Red Ribbon Fashion Gala 2012.

Mwakilishi wa Mohammed Dewji Foundation Bw. Cosmas Mtesigwa akinunua bidhaa za mnada zilizotoka kwa mmiliki
wa Kampuni ya Diamond Empowerment Fund Russel Simmons wa nchini
Marekani zenye thamani ya shilingi Milioni 5 ikiwa ni mchango wa
Mohammed Dewji Foundation kwa kituo cha watoto yatima cha TMH.

Mh. Zitto Kabwe akionyesha kitabu ‘SUPER RICH’ kilichoandikwa na Russel Simmons alichonunua kwa thamani ya Shilingi Milioni 4 kama mchango wake kwa kituo
cha watoto yatima kinachoongozwa na Mwanamitindo Khadija Mwanamboka cha
TMH. Kushoto ni Mwanamitindo wa Kimataifa Mtanzania anayeishi nchini
Marekani aliyekuja na bidhaa hizo Flaviana Matata.
Flaviana
Matata akiwaonyesha wageni baadhi ya bidhaa alizokuja nazo kutoka
kwenye kampuni ya Diamond Empowerment Fund ya Russel Simmons ya nchini
Marekani ambao ni mchango wa mfanyabiashara huyo wa kimataifa kwa kituo cha TMH.

Mh. Zitto Kabwe na Chief Judge wa BSS Madam Ritha Paulsen katika Meza kuu.

Flaviana Matata na Eve Collection.

Mwakilishi
wa Kampuni ya MeTL Cosmas Mtesigwa (kulia) Operation Manager wa Mo Blog
Johary Kachwamba na Assistant Operation Manager Zainul Mzige nao
waliokuwa miongoni mwa wageni waalikwa.


Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mabibo Beer Wines & Spirits Ltd
Bi. Benedicta Rugemalira akiwa na binti yake mmiliki wa Eve Collection.


Mh, Zitto Kabwe sambamba na msanii Linex wakichana mistari ya wimbo wa Lekadutigite katika hafla hiyo.

Hafla
hiyo ilipochanganya…… Shose Sinare naye alishindwa kujizuia na kujiunga
na Mh. Zitto Kabwe na Msanii Linex katika Lekadutigite.

Tharaia Ahmed wa CFAO MOTORS (katikati) akishow love na wadau.

Mc Abby Plaatjes na wadau.

