photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> > SHEREHE YA MIAKA 20 YA KLAB BILLICANAS NA 13 YA CLOUDS FM KWA PAMOJA

SHEREHE YA MIAKA 20 YA KLAB BILLICANAS NA 13 YA CLOUDS FM KWA PAMOJA

Posted on Dec 3, 2012 | No Comments

Sherehe hizo zilipambwa na shamrashamra za aina mbalimbali ikiwemo kukati keki pamoja na kufungua shampeni.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bilicanas Group Dk. Lilian Mtei akizungumza katika hafla hiyo.
Mwakilishi wa Clouds FM, Wasiwasi Mwabulambo akizungumza katika hafla hiyo.
Dk. Lilian Mtei akikata keki.
 Mmoja kati ya wafanyakazi wa kwanza wakati Bilicanas Club inaanzishwa miaka 20 iliyopita, Monika Victor akimlisha keki, Dk. Lilian Mtei wakati wa hafla ya kutimiza miaka 20 ya klabu hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
 Monica Victor akigawa keki kwa wadau waliofika katika sherehe hizo.
Mkurugenzi wa ASET, Asha Baraka akiwa na mmiliki wa blog ya Bongoweekend, Khadija Kalili pamoja na wadau wengine.
Bendi ya muziki ya dansi ya Sky Light ikitumbuiza katika sherehe za kutimiza miaka 20 ya Club Bilicanas na miaka 13 ya Clouds FM.
Watu wa mataifa mbalimbali wakicheza muziki katika ukumbi wa Bilicanas.
Wadau mbalimbali wa burudani  wamefurahia kwa pamoja  na kula keki ya miaka 20 ya klabu ya Kimataifa ya Bilicanas na miaka 13 ya Clouds Fm,  iliyoambatana na shamrashamra mbalimbali ndani  na nje ya  ukumbi huo.
Sherehe hizo ziliongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Bilicanas Group Dkt. Lilian Mtei  ambapo amewashukuru wadau hao kwa kuwa bega kwa bega na klabu hiyo, tangu 1992.
Amesema “Tunawashukuru sana kwa kuwa nanyi mara zote inatia faraja kwetu na tutaendelea kutoa huduma bora siku zote”.
Dkt. Mtei pia amewashukuru wafanyakazi mbalimbali waliofanikisha ukumbi huo kufikia hapo na kutoa heshima ya kipekee kwa wafanyakazi  waliokuwapo  tokea inaanza hadi ilipofikia miaka 20 na hatimaye  kukata keki hiyo.
“Uwepo wa miaka 20, tuna kila sababu ya kuwapongeza wafanyakazi  tuliokuwa nao toka mwanzo hadi sasa, na kwa heshima ya pekee  Mama Victor na Mrs. Mitemo  ndiyo watakao kata keki hii” alisema. Mtei.
Keki hiyo ilikatwa na wafanyakazi   hao  Monica  Victor na Pili Mitemo  ambaye alimwakilisha mumewe aliyekuwa Meneja wa kwanza wa klabu hiyo, ambaye kwa sasa ni marehemu.
Aidha, kwa upande wa Clouds FM, iliwakilishwa na Wasiwasi Mwabulambo ambaye alipongeza klabu Bilicanas kwa kuwa mstari wa mbele katika kuinua sanaa nchini hasa kwa kuwasaidia wasanii kufikia malengo yao.
Kwa upande wake Ibrahim Tuwa ‘Dj Ibra’ aliyekuwa akisherehesha  shughuli hiyo, aliwaomba wadau kuendelea kuwaunga mkono na kuwa wataendelea na huduma bora zaidi ya hapo.
Dj Ibra alijiunga na Bilicanas tokea 2002, ambapo mpaka sasa ana miaka 10 kwenye klabu hiyo  iliyowahi kuwa na madj maarufu waliopita  hapo ambao wengi wao wapo kwenye vituo vya televisheni na redio.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru