photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> > Mata ajasiliwa na Manchester United

Mata ajasiliwa na Manchester United

Posted on Jan 22, 2014 | No Comments



Juan Mata

Ombi la Manchster United la kutaka kumsajili nyota wa Chelsea Juan Matata imekubalika.

Ripoti zinasema United imetumia takriban kitita cha pauni milioni 37 kumsajili mcheza kiungo huyo wa Chelsea.


Mata mwenye umri wa miaka 25, anatarajiwa kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu baadaye hii leo, kabla ya kukamilisha usajili huo.

Mchezaji huyo kutoka Uhispania anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka minne na nusu na klabu hiyo iliyo na makao yake katika uwanja wa Old Trafford.

Mata ambaye aliichezea Chelsea, mechi 32, aliwaaga wachezaji wenzake na wakufunzi wa Chelsea katika uwanja wao wa mazoezi wa Cobham siku ya Jumatano.
Manchester United yakana fununu


Kocha wa Manchester United David Moyes

Awali kulikuwa na fununu kuwa Mata mwenye umri wa miaka ishirini na mitano, alitaka kuondoka kutoka Chelsea, baada ya kushinda kupata nafasi miongoni mwa wachezaji wa kwanza kumi na mmoja wa Chelsea, chini ya kocha wao mpya Jose Mourinho.

Siku ya Jumanne, Chelsea ilitangaza kuwa hawana nia yoyote ya kumuuza nyota wake Mata, ambaye aliteuliwa kuwa mchezaji bora wa klabu hiyo mwaka uliopita.

Lakini mchezaji huyo ambaye alikuwa kikosi cha Uhispania kilichoshinda kombe la dunia mwaka wa 2012, aliondolewa katika mechi tisa kati ya kumi na tatu alizocheza za ligi kuu ya premier msimu huu, hali iliyozua fununu kuwa huenda akauzwa mwezi huu wa Januari.

Kwingineko klabu ya Cardif inatarajia kumsaini mchezaji wa Manchester United Wilfred Saha kwa mkopo hadi mwisho wa msimu huu.

Zaha mwenye umri wa miaka ishirini na moja alifanyiwa uchunguzi wa matibabu siku ya Jumatano na Cardiff inataka kukamilisha usajili huo kabla ya mechi yao ya raundi ya nne ya kuwania kombe la FA dhidi ya Bolton.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru