Mwenge wa Uhuru wakimbizwa Wilayani Namtumbo.
Posted on
Jun 1, 2012
|
No Comments
Mtoto Mezea Seif wa darasa la kwanza katika shule ya msingi Njalamatata akiwa ameshika Mwenge wa Uhuru wakati ulipokuwa katika kijiji hicho wilaya ya Namtumbo kwa kazi ya kuhimiza shughuli za maendeleo jana.
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kapteni Honest Mwanossa akizindua mradi wa kisima cha maji safi ya kunywa kwa ajili ya wanafunzi wa shule ya sekondari ya Utwango wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma.Kulia ni Mbunge wa jimbo la Namtumbo Vita Kawawa.
Raia wa Marekani aliyefahamika kwa jina moja la Penzia akiwa ameshika Mwenge wa Uhuru wakati uliposimama katika kijiji cha Hanga kutoa ujumbe kwa wananchi kuhusu umuhimu wa wananchi kujiandaa kuhesabiwa ifikiapo Agosti 26,2012.
