photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> > SHULE YA SEKONDARI YA OLASITI YAKABIDHIWA MSAADA WENYE THAMANI YA SHILINGI MILLION 7

SHULE YA SEKONDARI YA OLASITI YAKABIDHIWA MSAADA WENYE THAMANI YA SHILINGI MILLION 7

Posted on Jun 26, 2012 | No Comments

SHULE ya sekondari ya Olasiti iliyopo katika kata hiyo  jijini Arusha,
imeondokana na changamoto kubwa iliyokuwa ikiwakabili kwa kipindi cha
muda mrefu ya ukosefu wa madawati iliyosababisha wanafunzi kukalia ndoo
na mawe, hali ambayo iliwalazimu  wadau mbalimbali wa elimu kujitokeza
nakusaidia  viti mia mbili na meza zake.
Msaada huo umetolewa hivi karibuni na Alex Martin ambaye
ni mfanyabiashara wa jijini hapa na kuukabidhi kwa uongozi wa kata hiyo
(ODC)mbele ya  mkuu wa shule hiyo,Paulina Alex Bagoye ambapo msaada huo
umeweza kupunguza changamoto kubwa iliyokuwaikiwakabili wanafunzi wa
shule hiyo kwa muda mrefu.
Akizungumza wakati wa kukabithi msaada huo, Mfanyabiashara huyo,
alisema kuwa alifikia hatua ya kutoa meza na viti mia moja  ambavyo
vina thamani ya  shs  7milioni kwa shule hiyo ambapo awamu ya kwanza
aliwahi kusaidia viti nameza  hamsini vyenye thamani ya shs  3.5
milioni huku lengo likiwa ni kuwawezeshawanafunzi kuweza kusoma katika
mazingira mazuri na hatimaye kuongeza ufaulu wa masomo.
Alisema kuwa, shule hiyo imekuwa ikikabiliwa na changamotohiyo
kutokana na upya kwani kabla ya hapo kata hiyo ilikuwa haina shule
yasekondari hali ambayo ilikuwa ikiwalazimu  wanafunzi kutembea umbali
mrefu wa zaidi yakilometa  kumi na tano kufuata elimu yasekondari
katika shule ya Oljoro iliyopo kata ya Terat jijiji hapa.
Aliongeza kuwa, hatua ya wanafunzi hao kusoma wakikalia ndoona mawe
imekuwa ikichangia kwa kiasi kikubwa sana kutofanya vizuri kimasomo
kwawanafunzi hao kwani walikuwa wakisoma katika mazingira magumu sana,
hivyo halihiyo ilimlazimu kutafuta jitihada mbalimbali kwa
kuwashirikisha marafiki nawadau mbalimbali katika kumuunga mkono
kuisaidia shule hiyo.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru