SHULE YA SEKONDARI YA OLASITI YAKABIDHIWA MSAADA WENYE THAMANI YA SHILINGI MILLION 7
Posted on
Jun 26, 2012
|
No Comments
SHULE ya sekondari ya Olasiti iliyopo katika kata hiyo jijini Arusha,
imeondokana na changamoto kubwa iliyokuwa ikiwakabili kwa kipindi cha
muda mrefu ya ukosefu wa madawati iliyosababisha wanafunzi kukalia ndoo
na mawe, hali ambayo iliwalazimu wadau mbalimbali wa elimu kujitokeza
nakusaidia viti mia mbili na meza zake.
Msaada huo umetolewa hivi karibuni na Alex Martin ambaye
ni mfanyabiashara wa jijini hapa na kuukabidhi kwa uongozi wa kata hiyo
(ODC)mbele ya mkuu wa shule hiyo,Paulina Alex Bagoye ambapo msaada huo
umeweza kupunguza changamoto kubwa iliyokuwaikiwakabili wanafunzi wa
shule hiyo kwa muda mrefu.
Akizungumza wakati wa kukabithi msaada huo, Mfanyabiashara huyo,
alisema kuwa alifikia hatua ya kutoa meza na viti mia moja ambavyo
vina thamani ya shs 7milioni kwa shule hiyo ambapo awamu ya kwanza
aliwahi kusaidia viti nameza hamsini vyenye thamani ya shs 3.5
milioni huku lengo likiwa ni kuwawezeshawanafunzi kuweza kusoma katika
mazingira mazuri na hatimaye kuongeza ufaulu wa masomo.
Alisema kuwa, shule hiyo imekuwa ikikabiliwa na changamotohiyo
kutokana na upya kwani kabla ya hapo kata hiyo ilikuwa haina shule
yasekondari hali ambayo ilikuwa ikiwalazimu wanafunzi kutembea umbali
mrefu wa zaidi yakilometa kumi na tano kufuata elimu yasekondari
katika shule ya Oljoro iliyopo kata ya Terat jijiji hapa.
Aliongeza kuwa, hatua ya wanafunzi hao kusoma wakikalia ndoona mawe
imekuwa ikichangia kwa kiasi kikubwa sana kutofanya vizuri kimasomo
kwawanafunzi hao kwani walikuwa wakisoma katika mazingira magumu sana,
hivyo halihiyo ilimlazimu kutafuta jitihada mbalimbali kwa
kuwashirikisha marafiki nawadau mbalimbali katika kumuunga mkono
kuisaidia shule hiyo.
imeondokana na changamoto kubwa iliyokuwa ikiwakabili kwa kipindi cha
muda mrefu ya ukosefu wa madawati iliyosababisha wanafunzi kukalia ndoo
na mawe, hali ambayo iliwalazimu wadau mbalimbali wa elimu kujitokeza
nakusaidia viti mia mbili na meza zake.
Msaada huo umetolewa hivi karibuni na Alex Martin ambaye
ni mfanyabiashara wa jijini hapa na kuukabidhi kwa uongozi wa kata hiyo
(ODC)mbele ya mkuu wa shule hiyo,Paulina Alex Bagoye ambapo msaada huo
umeweza kupunguza changamoto kubwa iliyokuwaikiwakabili wanafunzi wa
shule hiyo kwa muda mrefu.
Akizungumza wakati wa kukabithi msaada huo, Mfanyabiashara huyo,
alisema kuwa alifikia hatua ya kutoa meza na viti mia moja ambavyo
vina thamani ya shs 7milioni kwa shule hiyo ambapo awamu ya kwanza
aliwahi kusaidia viti nameza hamsini vyenye thamani ya shs 3.5
milioni huku lengo likiwa ni kuwawezeshawanafunzi kuweza kusoma katika
mazingira mazuri na hatimaye kuongeza ufaulu wa masomo.
Alisema kuwa, shule hiyo imekuwa ikikabiliwa na changamotohiyo
kutokana na upya kwani kabla ya hapo kata hiyo ilikuwa haina shule
yasekondari hali ambayo ilikuwa ikiwalazimu wanafunzi kutembea umbali
mrefu wa zaidi yakilometa kumi na tano kufuata elimu yasekondari
katika shule ya Oljoro iliyopo kata ya Terat jijiji hapa.
Aliongeza kuwa, hatua ya wanafunzi hao kusoma wakikalia ndoona mawe
imekuwa ikichangia kwa kiasi kikubwa sana kutofanya vizuri kimasomo
kwawanafunzi hao kwani walikuwa wakisoma katika mazingira magumu sana,
hivyo halihiyo ilimlazimu kutafuta jitihada mbalimbali kwa
kuwashirikisha marafiki nawadau mbalimbali katika kumuunga mkono
kuisaidia shule hiyo.

