KUTOKA VIWANJA VYA SABASABA..
Posted on
Jul 3, 2012
|
No Comments
Wateja wakipatiwa huduma.
Muonekano wa banda lao.
Programe Director wa Arti- Tanzania, Dennis Tessier akiwa ndani ya banda lao.
| Meneja wa mambo ya mkaa, Allan Shahidi akitoa somo kwa wateja waliofika bandani hapo. |
Maonesho ya 36 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam yanaendelea katika Viwanja vya Mwalimu JK Nyerere jijini Dar es Salaam ikikusanya pamoja wafanya biashara wakubwa kwa wadogo ambapo kati yao wapo Wauzaji wa Vipodozi wanaokuja kwa kasi kwa mali zao za uhakika AK Classic Cosmetics ambao wametoka Sinza Kumekucha kuja kuwaonesha na kuwauzia hapa sabasaba. Pichani ni Albert AK (katikati) akiwa na timu yake Ramadhani Alli na Rose Mmari.
Ramadhani Alli akiweka sawa bidhaa. Ukikutana na Father Kidevu ananukia ujue ni mambo ya AK hayo.
Zipo bidhaa kibao ila wahi kabla SALE maalum ya Saba Saba haijaisha
Watu kibao...sasa wewe unangoja nini kufika hapa Banda la Ali Hassan Mwinyi kujipatia vitu vyako vya uhakika.
Mnakaribishwa sana na hizi zote ni zenu piteni tu AK Classic Cosmetics mjipatie kwa gharama nafuu.
DAIMA huwezi zungumzia bidhaa za maziwa bila kutaja bidhaa za ASAS Dairies IRINGA ambao huzalisha bidhaa za aina mbalimbali zitokanazo na Maziwa halisi ya Ng’ombe.
Maonesho ya 36 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam yanaendelea katika Viwanja vya Mwalimu JK Nyerere jijini Dar es Salaam ASAS DAIRIES wapo katika banda la KARUME fika hapo na ujipatie mahitaji yako ya Maziwa.
Bidhaa zimesheheni na vinavyostahili kuliwa vya Baridi utavipata baridi kwa fleva za kila namna
Wateja wakubwa kwa watoto wakijipatia bidhaa za maziwa bora kutoka banda la ASAS ndani ya Maonesho ya Saba Saba.
Karibuni katika Banda la Bodi ya Maziwa Tanzania na utawakuta ASAS DAIRIES kwa bidhaa bora za Maziwa.
Afisa wa Benki ya ACB, Irine Joseph akiwasikiliza wananchi walio tembelea banda la Benki hiyo lililopo katika viwanja vya Maonesho ya 36 ya Kimataifa ya biashara Dar es Salaam. ACB ipo ndani ya jingo la Karume.
Timu nzima ya ACB Bank iliyopo katika viwanja vya Sabasaba kutoa huduma
Wananchi mbalimbali wakisikilizwa na watoa huduma katika Banda la Benki ya ACB.












