MADAKTARI: MATE YAWEZA KUENEZA VIRUSI VYA UKIMWI
Posted on
Jul 8, 2012
|
No Comments
WATAALAMU wa afya nchini wamefafanua kuwa kuna uwezekano mate kuwa na virusi vya Ukimwi (VVU).Ufafanuzi huo umetolewa kufuatia watu wengi kukumbwa na utata baada ya ugunduzi wa hivi karibuni wa kipimo cha kutambua waathirika wa Ukimwi kwa kutumia ute unaopatikana katika kinywa. Watu mbalimbali waliokuwa na dukuduku hilo walipiga simu kwenye ofisi za gazeti hili baada ya kuripoti kuhusu Mamlaka ya Kudhibiti Chakula na Dawa Nchini Marekani(FDA), kuthibitisha na kupitisha matumizi ya kifaa hicho kinachojulikana kwa jina la OraQuick. Madaktari waliohojiwa na Mwananchi Jumapili walisema kuwa kipimo hicho hakipimi uwepo wa VVU kwenye mate bali aina maalumu ya chembe kinga zinazojulikana kwa jina la kitaalamu kama ‘antibodies’, ambazo huzalishwa na mwili baada ya virusi kuingia katika mwili wa binadamu. |
WATAALAMU wa afya nchini wamefafanua kuwa kuna uwezekano mate kuwa na virusi vya Ukimwi (VVU).
