photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> MADAKTARI: MATE YAWEZA KUENEZA VIRUSI VYA UKIMWI

MADAKTARI: MATE YAWEZA KUENEZA VIRUSI VYA UKIMWI

Posted on Jul 8, 2012 | No Comments

WATAALAMU wa afya nchini wamefafanua kuwa kuna uwezekano mate kuwa na virusi vya Ukimwi (VVU).
Ufafanuzi huo umetolewa kufuatia watu wengi kukumbwa na utata baada ya ugunduzi wa hivi karibuni wa kipimo cha kutambua waathirika wa Ukimwi kwa kutumia ute unaopatikana katika kinywa.

Watu mbalimbali waliokuwa na dukuduku hilo walipiga simu kwenye ofisi za gazeti hili baada ya kuripoti kuhusu Mamlaka ya Kudhibiti Chakula na Dawa Nchini Marekani(FDA), kuthibitisha na kupitisha matumizi ya kifaa hicho kinachojulikana kwa jina la OraQuick.
Madaktari waliohojiwa na Mwananchi Jumapili walisema kuwa kipimo hicho hakipimi uwepo wa VVU kwenye mate bali aina maalumu ya chembe kinga zinazojulikana kwa jina la kitaalamu kama ‘antibodies’, ambazo huzalishwa na mwili baada ya virusi kuingia katika mwili wa binadamu.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru