USIKU WA MTU MZIMA DAWA WAFANA JIJINI MWANZA INBOX
Posted on
Jul 7, 2012
|
No Comments

Wanaumeeee...eeeeeh..! Wanauuumeeeee.....halafu mashabiki wanaitikia kwa nguvu kabisa eeeehhhh..!

"Sijui nimtawanyee.....aah huwezi wewe mtu mzima dawa."! Mh Temba akikamua vilivyo na Bibi Cheka jukwaai saafi kabisa huku shangwe zikiwa zinasikika kila kona,kwani Bibi Cheka alionesha uwezo wake mkubwa wa kukamua jukwaa,hata ile mitindo huru nini na niniii yuko swafi mbaya..aaah mbona palinoga Villa Park usiku wa kuamkia leo.

Ommy Dimpoz akikamu mbele ya umati mkubwa ndani ya kiota cha maraha cha Villa Park usiku wa kuamkia leo.

Pamoja na kupotea kiaina kwenye gemu ya muziki wa Bongofleva,Ferouz bado nyota yake inaonekana kuwa angavu,alifanya vyema ndani ya ukumbi wa Villa Park,kiasa kwamba shangwe kila wakati zilikuwa za kutosha.

Mkubwaa na wanaweee....na yeyeee yumooo.. ! Mkubwa Fella nae akitafuta kimwana wa kunogesha jukwaa safi kabisa.

Mkali mwingine wa mitindo huru,Mwana FA a.k.a Binadamu akikamua vilivyo ndani ya ukumbi wa Villa Park usiku wa kuamkia leo,kwenye shoo ya usiku wa mkubwa dawa ambao ulifana kwa kiasi kikubwa.Picha zote Zimeletwa hapa na Michuzijr
