KIONGOZI WA KUNDI LA UAMSHO SHEIKH FARID NA BAADHI YA WAFUASI WAKE WAFIKISHWA MAHAKAMANI LEO.
                              Posted on 
                              Oct 22, 2012
                            |
                            
                                  No Comments
                                  

Gari
 la Polisi la pili ambalo liliwachukuwa Viongozi wa Jumuiya ya UAMSHO 
ambao walishitakiwa kwa makosa ya kufanya fujo na uchochezi likiwa 
linasindikizwa na magari ya Polisi kuja Mahakama ya Wilaya ya 
Mwanakwerekwe.

Askari
 wa kikosi cha kutuliza ghasia wakiwa wanaimarisha usalama katika eneo 
la Mahakama ya Wilaya Mwanakwerekwe ambapo Viongozi wa Jumuiya ya UAMSHO
 walipelekwa kwenda kusomewa mashitaka yao.


Mmoja
 kati ya Viongozi wa UAMSHO Shekh Azan Khalid Hamdan (43) akishuka 
kwenye gari la Polisi kuelekea Mahakamani Mwanakwerekwe kwenda kusomewa 
mashtaka yao.

Kiongozi
 wa Jumuiya ya UAMSHO Shekh Farid Hadi Ahmed akishuka kwenye gari la 
Polisi kuelekea Mahakama ya Mwanakwerekwe kwenda kusomewa mashtaka yao 
yanayomkabili ikiwemo kusababisha fujo na uchochezi.

Gari
 la Polisi ambalo liliwachukuwa Viongozi wa Jumuiya ya UAMSHO ambao 
walishitakiwa kwa makosa ya kufanya fujo na uchochezi likiwa linawasili 
Mahakama ya Wilaya ya Mwanakwerekwe.Viongozi hao wote walirudishwa rumande.(Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar).

 
 
 
 
 
 
 
 
