photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> > MAJADILIANO YA KUISAIDIA TANZANIA KIUCHUMI YAENDELEA JAPAN.

MAJADILIANO YA KUISAIDIA TANZANIA KIUCHUMI YAENDELEA JAPAN.

Posted on Oct 12, 2012 | No Comments

Ujumbe kutoka Tanzania ukiongozwa na Mhe. Waziri wa Fedha Dr. William Mgimwa pamoja na maafisa kutoka Benki ya Dunia wakiendelea na majadiliano juu ya kuangalia uwezekano wa kuisaidia Tanzania ili iweze kuendelea kiuchumi hapa Jijini Tokyo- Japan.
Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. William Mgimwa akiwa na ujumbe katika mkutano, wa kwanza kulia ni Bi. Salome Sijaona ambaye ni Balozi nchini Japan akifuatiwa na Bw. Siyvacius B. Likwelile Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha akifuatiwa na Bw. Khamisi Mussa Omari Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Zanzibar katika mkutano Jijini Tokyo- Japan.
Wa pili kutoka kulia ni Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia  kwa Bara la Afrika, Bw. Makhtar Diop,akiwa ameambatana na Maafisa  Waandamizi kutoka Benki ya Dunia wakati wa mazungumzo na Waziri wa Fedha Mhe. William  Mgimwa hayupo kwenye picha.
Wa kwanza kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Japan  Bi. Salome Sijaona akifuatiwa na Dk. Servacius B. Likwilile Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha akifuatiwa na  ni Mhe. Waziri wa Fedha Dr. William Mgimwa na  Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Zanzibar Bw. Khamis Mussa Omari walioko nyuma ni maafisa waandamizi  wa Tanzania Jijini Tokyo – Japan wakimsikiliza kwa makini Bw. Makhtar Diop, ambaye ni Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia kwa Bara la Afrika.
Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia  kwa Bara la Afrika, Bw. Makhtar Diop,akiwa ameambatana na  Maafisa  Waandamizi kutoka Benki ya Dunia wakati wa mazungumzo na Waziri wa Fedha Mhe. William  Mgimwa ambaye yuko na ujumbe wake kutka Tanzania pamoja na Balozi wa  Tanzania nchini Japan Bi. Salome Sijaona  katika kikao cha pamoja cha ambacho Mheshimiwa Waziri alikutana na Kiongozi huyo kwa madhumuni yakutoa mapendekezo ya maeneo ambayo Tanzania tukisaidiwa tutasonga mbele kiuchumi.
Kushoto kwa Gavana wa Benki Kuu Prof. Benno Ndulu ni Maafisa kwa Benki ya Dunia wakifuatilia kwa makini kuhusu mkutano huo wakiwa pamoja na ujumbe kutoka Tanzania hapa Jijini Tokyo – Japan.
Waziri wa fedha Mhe. Mgimwa akifafanua jambo kwa Afisa wa Benki ya Dunia.
Gavana wa Benki Kuu Profesa Benno Ndulu akitoa maoni yake  kwenye mkutano na Makamu wa Rais wa Dunia hayupo pichani hapa Jijini Tokyo- Japan.
Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia  kwa Bara la Afrika, Bw. Makhtar Diop akifurahia jambo wakati wa mazungumzo na Waziri wa Fedha Mhe. William  Mgimwa hayupo kwenye picha.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru