photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> > MAELFU WAFURIKA KIBANDAMAITI KUPONGEZA SAFU MPYA YA UONGOZI WA CCM.

MAELFU WAFURIKA KIBANDAMAITI KUPONGEZA SAFU MPYA YA UONGOZI WA CCM.

Posted on Nov 18, 2012 | No Comments

 Makamu Mwenyekiti  wa CCM (Bara), Rais wa Zanzibar  Dk. Ali Mohamed Shein akiingia uwanjani wa Kibandamaiti, Wilaya ya Mjini, wakati wa sherehe za Wana-CCM Zanzibar kuipongeza safu mpya ya uongozi. Kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Watatu Naibu Katibu Mkuu (Bara) Vuai Ali Vuai.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiingia Uwanja wa Kibanadamaiti katika sherehe ya wana-CCM wa Zanzibar kupongeza safu mpya ya uongozi wa CCM Taifa. Wengine ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Vuai Ali Vuai, Naibu Katibu Mkuu (Bara) Mwigulu Nchemba na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye.
Mamia ya wana-CCM Uwanja wa Kibandamaiti, wakati wa sherehe za wana-CCM wa Zanzibar kuipongeza safu mpya ya uongozi wa CCM Taifa.
Makatibu wa NEC, Mohamed Seif Khatib (Oganaizesheni) na Asha-Rose Migiro (Siasa na Mambo ya Nje) wakiteta jambo wakati wa mkutano wa wana-CCM Zanzibar kuipongeza safu mpya ya uongozi wa CCM Taifa, kwenye viwanja vya Kibandamaiti, mkoa wa mjini.
Vijana wa CCM wakishangilia kwa mtindo wa aina yake wakati wa sherehe hizo (Picha zote na Bashir Nkoromo).
Wakiserebuka.
Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Sheni akihutubia mamia ya Wana-CCM Kwenye Viwanja Vya  Kibanda Maiti, Mkoa Wa Mjini, Mjini Zanzibar katika Sherehe ya Wana-CCM Zanzibar kupongeza Safu mpya ya Uongozi wa CCM Taifa. (Picha Na Bashir Nkoromo).

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru