photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> > MLIPUKO ULIOUA WATU 7 KENYA WASABABISHA TAFRANI, WASOMALI WAPIGWA POLISI WAFYATUA RISASI.

MLIPUKO ULIOUA WATU 7 KENYA WASABABISHA TAFRANI, WASOMALI WAPIGWA POLISI WAFYATUA RISASI.

Posted on Nov 19, 2012 | No Comments

Abiria wasiopungua 7 waliuwawa jana na wengine zaidi ya 33 kujeruhiwa wakati  dalala ‘matatu’ iliyokuwa njiani kuelekea Kariobangi  ikitokea jijini Nairobi iliposhambuliwa kwa bomu katika kitongoji cha Eastleigh, katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi.
 Mkuu wa jeshi la polisi katika mkoa wa Nairobi, Moses Ombati, amesema walioshuhudia tukio hilo walimuona mtu akishuka kutoka kwenye matatu hiyo na kujaribu kuingia matatu nyingie iliyokuwa nyuma lakini akaanguka na kushambuliwa na umma. Ombati amesema hawana hakika kama mtu huyo alihusika na shambulizi hilo lakini wanafanya uchunguzi wa kina.
Dakika chache baadae vijana waliokuwa na hasira waliwalenga watu wa jamii ya Kisomali kwenye mtaa huo, Polisi ilibidi kufyatua risasi hewani kuwatawanya watu.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru