photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> > MOSHI MWEUSI VATICAN, BADO HAKUNA PAPA

MOSHI MWEUSI VATICAN, BADO HAKUNA PAPA

Posted on Mar 13, 2013 | 3 Comments



Moshi mweusi Vatican
Moshi mweusi umetokea kwenye dari la hekalu ya Sistine mjini Roma, kumaanisha kuwa makadinali walioko ndani ya hekalu wameshindwa kuafikiana juu ya Papa mpya anayetarajiwa kuchaguliwa.
Moshi mweupe utaashiria kupatikana kiongozi mpya wa kanisa Katoliki la Roma.
Makadinali hao wanatarajiwa kupiga kura mara nne kwa siku hadi pale thuluthi mbili ya makadinali wote watakapoafikiana juu ya Papa mpya.
Walipiga kura yao ya kwanza ambayo haikuleta maafikiano hapo usiku wa Jumanne. Yeyote atakayeteuliwa kuliongoza kanisa hilo katoliki anakabiliwa na wakati mgumu, ambapo kanisa limezongwa na kashfa mbali mbali pamoja na migawanyiko ya ndani.
Papa aliyeondoka Benedikt wa Kumi na sita aliwashangaza wengi alipotangaza kujiuzulu wadhifa huo miaka minane tu tangu kuchaguliwa. Yeye ndiye Papa wa kwanza kujiuzulu katika miaka 600 ya historia ya kanisa hilo.
Alitoa sababu kuwa amezeeka na afya yake imedhoofika kwa hivyo haoni kuwa anaweza kutekeleza wajibu wake kikamilifu kama Papa wa kanisa.

Comments: 3

  1. I am sure this paragraph has touched all the internet people,
    its really really nice piece of writing on building up new weblog.


    Feel free to visit my blog post ... no deposit casino bonuses

    ReplyDelete
  2. My name's Susannah from Zwijndrecht, Netherlands and I have to say your article is really informative. The clarity of your post is rather nice and I can trust you are an authority on this subject. With your approval, would you allow me to grab your RSS feed to keep up-to-date with forthcoming posts? Thanks a million and please carry on the fantastic work.

    Also visit my homepage ... americas next top model

    ReplyDelete
  3. I'm a writer from Georgenberg, Austria just sent this onto a coworker who is performing some research on this. And she in fact bought me lunch just because I came across it for her... lol. So allow me to paraphrase this.... Thanks for the meal... But anyways, thanks for taking some time to write about this issue here on your blog.

    Here is my web blog: toekomst

    ReplyDelete