photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> > USHABIKI UNAVYOWATESA VIJANA KATIKA SIASA

USHABIKI UNAVYOWATESA VIJANA KATIKA SIASA

Posted on Jan 23, 2014 | 1 Comment




Vijana wafuasi wa Chadema wakipigana mahakamani kutetea makundi wanayounga mkono.



KWA UFUPI

Mwamko huo kwa vijana umeendelea kukua kwa kasi mpaka sasa kupitia uhamasishaji wa makundi mbalimbali ya wanaharakati, wasomi na huo ukawa ni mwanzo wa baadhi ya vyama vya siasa kuona umuhimu wao, hivyo kila chama kuwavuta upande ke kwa maslahi yake.

Dar es Salaam. Mwamko wa vijana katika siasa ulianza kujitokeza katika kipindi cha uchaguzi wa mwaka 1995. Chama Cha Mapinduzi (CCM) mbali na mwamko wa vijana ulioibuka ndani yake, pia kilianza kupata upinzani mkali na kutupiwa lawama na kila aina ya kejeli kwa madai ya viongozi wake kukosa sifa za kuongoza nchi.


Mwamko huo kwa vijana umeendelea kukua kwa kasi mpaka sasa kupitia uhamasishaji wa makundi mbalimbali ya wanaharakati, wasomi na huo ukawa ni mwanzo wa baadhi ya vyama vya siasa kuona umuhimu wao, hivyo kila chama kuwavuta upande ke kwa maslahi yake.


Idadi kubwa kati ya vijana hao ni wahitimu wa vyuo mbalimbali na walioko vyuo vikuu ambao ni rahisi kupokea agenda za vyama husika na kuziendeleza, hivyo kutimiza malengo ya vyama husika.


Pamoja na hao, wapo vijana wenye elimu ya wastani, na wengine walioikosa kabisa, ambao ni rahisi kufanya lolote bila kujali matokeo yake, kwa kuwa wao ni ‘bendera fuata upepo’.


Kwa hali ya siasa ilivyo nchini, baadhi ya vijana wameanza kujikuta njiapanda, wakishindwa kuchagua ni chama gani, mwanasiasa yupi au kundi lipi linaweza kuwa tumaini jipya kwao.


Hatua hiyo inatokana na udhaifu unaoendelea kuonekana ndani ya vyama vya siasa, hususani vile vyenye ushindani mkubwa katika kipindi fulani – kama ilivyokuwa kwa NCCR na CCM mwaka 1995; CCM vs CUF mwaka 2000; na CCM vs Chadema mwaka 2010 na sasa tunapoelekea 2015.


Sote ni mashuhuda wa mivutano iliyopo, vurugu na tuhuma mbalimbali za mara kwa mara zisizokuwa na majibu.


Vuguvu hilo la vijana limeanza kuingia hata ndani ya vyama vyewenye, mfano ni katika uchaguzi wa Umoja wa Vijana wa CCM mwaka juzi, na hivi karibuni katika sakata la Chadema dhidi ya Zitto Kabwe.


Katika matukio hayo, tumeshuhudia jinsi vijana walivyoamua kupigana wao kwa wao, kila upande ukitaka kutimiza malengo yake.


Kutokana na mazingira hayo, wachambuzi wa masuala ya kisiasa nchini wanaeleza mitazamo mbalimbali inayosababisha vijana kuathiriwa na mapenzi ya vyama, au watu binafsi ndani ya vyama hivyo mpaka kufikia hatua ya kukosa uvumilivu, wakiamini kuwa chama hicho au watu hao ndio suluhisho la matatizo yao.

Comments:1