BREIVIK MTUHUMIWA WA MAUAJI NORWAY AHUKUMIWA MIAKA 21 JELA..
Posted on
Aug 24, 2012
|
No Comments
Mahakama ya Norway imeamua kuwa Anders Behring Breivik ana akili zake timamu, na imemhukumu kifungo cha miaka 21 kwa kuuwa watu 77 mwezi wa Julai mwaka jana.
Breivik siku zote amekiri kufanya mashambulio ya mabomu na bunduki, bila ya kuonesha majuto.Upande wa mashtaka ukitaka kupata uamuzi juu ya akili ya Breivik, na angekutikana punguani angewekwa kwenye jela ya wendawazimu kwa muda usiojulikana.
Amekuwa akishikilia kuwa ana akili yake, na kwamba aliyofanya ni vitendo vya kisiasa.
Alitabasamu hukumu ilipotolewa.
Wakili wa Breivik amethibitisha kuwa mteja wake hataomba rufaa.