photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> > MITETEMEKO YA IRAN YAUWA MAMIA YA WATU

MITETEMEKO YA IRAN YAUWA MAMIA YA WATU

Posted on Aug 12, 2012 | No Comments

Idadi ya watu waliokufa kwenye mitetemeko miwili ya ardhi nchini Iran inazidi kuongezeka, na sasa inajulikana kuwa watu kama 250 wamekufa.
Shughuli za uokozi baada ya mitetemeko ya Iran
Watu wengine 2,000 wamejeruhiwa.
Waokozaji wanawatafuta manusura kwenye kifusi cha majengo yaliyoporomoka katika miji na vijiji kwenye eno la mji wa Tabriz, kaskazini-magharibi mwa nchi.
Shirika la Mwezi Mwekundu la Iran limechukua uwanja wa mpira kuwapa hifadhi watu waliopoteza makaazi yao, au wanaogopa kurudi nyumbani.
Shirika hilo limetoa mahema, mablanketi na chakula.
Shirika la Mwezi Mwekundu la Uturuki, limesema linatuma msaada mpakani.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru