photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> > PICHA ZA YANGA NDANI YA IKULU RUWANDA

PICHA ZA YANGA NDANI YA IKULU RUWANDA

Posted on Aug 24, 2012 | No Comments

Mabingwa wa klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati timu ya Young Africans Sports Club, jana jioni ilitembelea Ikulu kuonana na Rais Paul Kagame, kufuatia mwaliko wa rais huyo wa Rwanda.
Ikiongozwa na mwenyekiti wa Young Africans Sports Club Yusuph Manji, iliwasili Ikulu ikiwa na wachezaji wake wote walioenda nchini Rwanda pamoja na viongozi wake.
Mchezaji mpya aliyesajiliwa kutoka APR Mbuyu Twite alikuwa miongoni mwa wachezaji  
waliohudhuria dhifa hiyo, ambapo Mwenyekiti wa bodi ya udhamini wa klabu Mama Fatma Karume na mjumbe wa bodi ya udhamini Seif Ahmed Magari walimkabidhi jezi ya Yanga rais Paul Kagame.
Kocha Mkuu wa Young Africans Tom Saintfiet na nahodha wake Nadir Haroub Cannavaro walimkabidhi kombe rais Kagame, kombe la klabu bingwa afrika mashariki CECAFA ambalo rais Kagame ndio mfadhili wake mkuu. 
Young Africans inashuka leo dimbani kucheza mchezo wa kirafiki na timu ya Rayon Sports.
YANGA wakiwa Kigali RwandaRais Paul Kagame wa Rwanda akiongea na Viongozi na wachezaji wa timu ya Young Africans walipomtembelea Ikulu.
Rais Paul Kagame akisalimiana na Mama Karume, mwenyekiti wa bodi ya udhamini wa klabu ya Young Africans.
Seif Ahmed Magari (kushoto) na Mama Fatma Karume wakimkabidhi jezi ya Young Africans rais Paul Kagame
Embedded image permalink

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru