AIR TANZANIA YAANZA TENA SAFARI ZAKE OKTOBA 12.
Posted on
Oct 10, 2012
|
No Comments
Inaonekana
Air Tanzania inafufuka taratibu. Jana kwenye facebook page ya kampuni,
wametoa taarifa ya kuanza safari mbalimbali hapa nchini wiki hii, na
wana mipango ya kuanza safari za nje miezi michache inayokuja. Taarifa
ya ATCL kutoka facebook inasema:
” Tunapenda kuwataarifu kuwa kuanzia Ijumaa, 12 Oktoba 2012,
tunarejesha upya huduma zetu za safari ambazo zilisitishwa kwa muda kwa
sababu zilizo nje ya uwezo wetu.
Tunaanza tena safari kati ya Dar es Salaam, Mwanza, na Kilimanjaro
siku hiyo, na kupanua wigo wa huduma zetu katika miezi ijayo.
Tunatarajia kuanza safari kuelekea Arusha na Zanzibar mwanzoni wa mwezi
Novemba, na safari za Mtwara na Moroni Hahaya baadaye mwezi huo.
Tunatarajia kusambaza huduma za safari hadi Dubai kabla ya mwisho wa
mwaka.
Tunawashukuru sana nyote kwa uvumilivu wenu na kwa kuendelea kutuunga mkono.
Tafadhali tembelea ofisi zetu au za wakala wa usafiri kufanya booking
kwa ajili ya kusafiri na Air Tanzania, The Wings of Kilimanjaro.”