photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> > PICHA ZA USHAHIDI ZAWAUMBUA MAPOLISI AFRIKA KUSINI.

PICHA ZA USHAHIDI ZAWAUMBUA MAPOLISI AFRIKA KUSINI.

Posted on Nov 7, 2012 | No Comments

Picha zilizowasilishwa mbele ya tume inayochunguza mauaji ya wachimba migodi waliouawa karibu na mgodi wa palatinum wa Marikana zinaonekana kudhibitisha tuhuma kuwa maafisa wa polisi nchini Afrika kusini  waliweka silaha karibu na miili.
Picha ya kwanza inaonyesha mwili wa mwanamume aliyefariki katika sehemu iliyo karibu na mgodi wa Marikana.
Picha ya pili iliyopigwa baadaye lakini siku hiyo hiyo, ni sawa na picha ya kwanza lakini hii inaonyesha mwanamume huyo huyo akiwa na panga lenye mkono wa rangi ya njano lililo chini ya mkono wake wa kulia.
Picha zote zilipigwa na maafisa wa polisi wa Afrika kusini muda mfupi tu baada ya kuuawa kwa wachimba mgodi thelathini na wanne na polisi mnamo mwezi Agosti.
Ipo mifano mingine zaidi na inamaanisha kuwa huenda eneo la tukio la uhalifu lilibadilishwa na maafisa hao wa polisi ili waweze  kujitetea kuwa waliwashambulia wachimba mgodi hao ili kujikinga.
Wakili George Bizos ambaye kwa wakati mmoja alimtetea Nelson Mandela, anasema kuna ushahidi mzito wa kujaribu kuzuia haki kutendeka na hivyo ametoa wito kwa maafisa wakuu wa polisi kueleza ni nini kilichotokea.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru