photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> > KIBAKI AHUTUBIA TAIFA LA KENYA KWA MARA YA MWISHO KAMA RAIS

KIBAKI AHUTUBIA TAIFA LA KENYA KWA MARA YA MWISHO KAMA RAIS

Posted on Dec 13, 2012 | No Comments

Sherehe za mwaka huu za uhuru wa Kenya zilzo fanyika jana tarehe 12 Desemba ni nafasi ya mwisho kwa Rais Mwai Kibaki kulihutubia taifa katika sikukuu ya kitaifa hasa ikizingatiwa sikukuu nyingine ya kitaifa ni Siku ya Madaraka itakayokuwa tarehe 1 Juni mwakani, ambapo atakuwa hayupo tena madarakani.
Kenya ilitumbukia katika ghasia zilizosababishwa na harakati za kuwania madaraka kati ya rais Mwai Kibaki na Raila Odinga baada ya uchaguzi mwaka 2008 kabla ya kufikiwa makubaliano yaliyosimamiwa na jopo maalum la Kimataifa lililoongozwa na katibu mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa Kofi Annan na hatimae kuundwa serikali ya muungano.
Machafuko baada ya uchaguzi wa mwaka 2007 yalisababisha kiasi ya watu 1,100 kuuwawa na wengine zaidi ya 65,000 kupoteza makaazi yao.
Ikiwa ni tukio lake la mwisho la kitaifa kuliongoza kabla ya kuondoka madarakani baada ya uchaguzi mkuu wa mwezi Machi mwaka 2013, Rais Mwai Kibaki ameitumi siku ya uhuru  kuzungumzia mafanikio yaliyopatikana nchini humo tangu alipoingia madarakani miaka 10 iliyopita, kubwa zaidi ikiwa ni ukuaji wa kiuchumi, maendeleo ya sekta ya miundo mbinu kutokana na miradi iliyoanzishwa katika kipindi hicho cha utawala wake pamoja na kupitishwa katiba mpya mwaka 2010
Katika hotuba  amewahimiza wananchi wa Kenya kutilia maanani umuhimu wa amani na usalama na kuweka kando tofauti za kikabila katika uchaguzi mkuu ujao huku pia akizungumzia juhudi za serikali katika kupambana na wanamgambo wa kundi la Al-Shabab nchini Somalia ambako jeshi la Kenya linashirikiana na kikosi cha Umoja wa Afrika katika harakati hizo.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru