photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> > MISRI IKULU HAIKALIKI...

MISRI IKULU HAIKALIKI...

Posted on Dec 6, 2012 | No Comments

Vurugu zimezuka katika mji mkuu wa Misri, Cairo, baina ya watu wanaomuunga mkono Rais wa taifa hilo Mohammed Mursi na wapinzani kufuatia kutangazwa kwa taarifa kuwa kura ya maoni inayohusu mswada wa katiba mpya itafanyika kama ilivyopangwa ifikapo tarehe 15 ya mwezi huu.
 Kauli hiyo iliyotolewa na makamu wa Rais wa Misri Mahmud Mekki, imesababisha vurugu kubwa nje ya Ikulu ambapo mahema yanayozunguka eneo hilo yaliangushwa. Waandamanaji wamewasha moto mitaani, kurusha mawe pamoja na mabomu ya petroli.
Maandamano ya kumpinga Rais Mursi yameikumba Misri tangu kiongozi huyo ajipe madaraka ya ziada wiki mbili zilizopita. Waandamanaji wamelazimika kuondoka nje ya Ikulu na maeneo ya jirani kutokana na hali ya mapigano kuwa mbaya zaidi.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru