photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> > RAIS WA VENEZUEKA APATA NAFUU

RAIS WA VENEZUEKA APATA NAFUU

Posted on Dec 13, 2012 | No Comments


Rais Hugo Chavez
Rais Hugo Chavez
Serikali ya Venezuela inasema hali ya rais Hugo Chavez inazidi kuimarika baada ya kufanyiwa upasuaji nchini Cuba Jumanne. Anaugua ugonjwa wa saratani.
Lakini mawaziri wamesema kwamba siku za usoni zitakuwa ngumu kwake na itachukua muda mrefu kwake kupona. Waliwaonya wananchi wa Venezuela wajitayarishe kwa siku za baadaye zenye hali ngumu.
Chavez, mwenye umri wa miaka 58, sasa amefanyiwa upasuaji mara nne tangu alipoanza kuugua mwezi Juni 2011.
Taarifa kuhusu ni saratani ipi inayomsumbua Chavez haijawahi kutangazwa hadharani.
Maombi
Rais Rafael Correa wa Ecuador, mshirika wa karibu wa Chavez, amesema ni sharti mifumo yake ya mabadiliko nchini Venezuela iendelee, hata kama hataweza kurejea mamlakani.
Televisheni ya taifa ilirusha picha zilizoonyesha wananchi wa Venezuela wakimuombea rais kanisani.
Chavez angali nchini Cuba, na haijulikani ni lini atarejea nchini. Anatarajiwa kuapishwa rasmi kwa muhula wake wa nne kama rais katika kipindi cha mwezi mmoja ujao.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru