photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> > WANAOMILIKI SILAHA KINYUME CHA SHERIA WAPEWA SIKU 30 KUZISALIMISHA

WANAOMILIKI SILAHA KINYUME CHA SHERIA WAPEWA SIKU 30 KUZISALIMISHA

Posted on Dec 6, 2012 | No Comments


 Serikali imetoa siku 30 kwa wananchi wanaomiliki silaha kinyume na sheria kuzisalimisha kabla hawajachukuliwa hatua za kisheria.
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dkt. Emmanuel Nchimbi (Pichani) wakati akizungumza na waandishi wa habari
Dkt. Nchimbi alisema kuwa na tatizo la kuzagaa na matumizi holela ya silaha zinazomilikiwa isivyo halali lichangia matukio ya uhalifu ambayo yamekuwa yakijitokeza  sehemu mbalimbali nchini
Alisema kuwa kwa mfano katika mwezi Januari hadi Septemba mwaka huu kumekuwepo na matukio ya ujambazi 876 ambayo yalisababisha vifo 138 vya raia na 6 vya askari.
Aidha Dkt . Nchimbi aliongeza kuwa  jumla ya mali zenye thamani ya shilingi  bilioni 4.5 zilizoibiwa kwa kutumia silaha zinazomilikiwa kinyume cha sheria na zile zinazomilikiwa kisheria lakini wamiliki wake wanazitumia katika uhalifu.
Aliongeza kuwa kipindi cha kuanzia Januari hadi Septemba mwaka huu jumla ya  silaha 62 ziliibiwa  kutoka kwa wamiliki wake halali na silaha 304 zilikamatwa katika matukio mbalimbali ya uhalifu
Kufuatia hali hiyo Serikali imewaagiza watu wote wanaomiliki silaha kinyume cha Sheria kusalimisha silaha hizo katika vituo vya Polisi au wenyeviti wa vitingoji , wakuu wa mikoa na wilaya.
Aidha Dk. Nchimbi alisema  kuwa kwa wale ambao muda utakamilika bila kusalimisha silaha msako mkali utafanyika kuanzia tarehe 5 Januari mwakani
Waziri Nchimbi aliwataka wananchi kushirikiana na vyombo vya dola kutoa taarifa zitakazosaidia kubaini uhalifu na makundi yaliyo katika jamii yetu.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru