photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> > ATIWA MBARONI KWA KUJIFANYA YEYE NI WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA UGANDA.

ATIWA MBARONI KWA KUJIFANYA YEYE NI WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA UGANDA.

Posted on Oct 16, 2012 | No Comments

Pichani ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Uganda Mh. Sam Kutesa.
Kijeba mmoja mwenye umri wa miaka 33 nchini Uganda ametiwa korokoroni na polisi nchini Uganda baada ya kujifanya yeye ni Waziri wa mambo ya Nje wa Uganda Sam Kutesa na kudai shilingi milioni 165 kwa muwekezaji mwenye asili ya Kiasia.
Jamaa huyo mfanyabiashara kutoka wilaya ya Wakiso mwenye umri wa miaka 33 Collins kato, ambaye pia hujulikana kwa jina la Moses Barigye amekamatwa mjini Kololo mjini Kampala na baadae kukabidhiwa kwa mikononi mwa polisi.
Kukamatwa kwa bw. Kato kunafuatia malalamiko ya Vasavada Asis mmiliki wa Kampuni ya Mara Group iliyopo Kololo, ambaye aliwataarifu maafisa usalama kuwa Kato amekuwa akimbugudhi na kudai fedha kutoka kwake.
Inadaiwa kuwa Bw. Kato alikuwa akimwambia muwekezaji Asis kuwa yeye kama Waziri anahitaji fedha kwa ajili ya ziara ya kikazi nje ya nchi kwenye mkutano wa kimataifa na kuwa atailipa kwa kumuunganishia mikataba poa ya za serikalini.
Kwa mujibu wa Msemaji wa Polisi wa Kampala Metropolitan Ibin Ssenkumbi, mfanyabiashara huyo aliingia kwenye mstari na kuwataka wafanyakazi wake kuweka fedha hizo kwenye mfuko na kumpelekea Kato.
Lakini machale yaliwacheza baadhi ya wafanyakazi hao waliokuwa na namba ya simu ya Mh. Waziri Kutesa na kuamua kumpigia na kumuuliza fedha hizo tukuletee wapi? Jambo lilimshtua na kushangaa fedha na za nini tena kutoka kwa naniii..???
Baada ya hayo taarifa ilifikishwa polisi, ambapo sasa wao walijifanya ni wafanyakazi wa Nara Group na kuwa wakutane wamkabidhi fedha zake, ambapo alipotia timu aliishia kucheza na pingu na sasa anajuta kujifanya waziri.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru