LIBYA INA MAELFU YA WAFUGWA
Posted on
Jul 14, 2012
|
No Comments
Wakuu wa Libya wanachagizwa kuchukua dhamana ya watu wanaokisiwa kuwa 5000, ambao wanazuwiliwa na makundi ya wanamgambo bila ya kufanyiwa mashtaka rasmi.
Shirika la kutetea haki za kibinaadamu, Human Rights Watch, linasema limeorodhesha kesi za watu ambao wameadhibiwa sana wakati wanazuwiliwa na wapiganaji hao wa zamani.
Human Rights Watch inasema, wengi kati ya wale wanaozuwiliwa ni wale waliokuwa wafuasi wa kiongozi wa zamani wa Libya, Moammar Gaddafi, kabla ya kupinduliwa mwaka jana.
Wakuu wa Libya wakitakiwa wawe wameshapeleka kesi zote hizo mahakamani, ilipofika tarehe 12 Julai.