photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> > MAREKANI YAIPA KENYA NDEGE ZA KISASA

MAREKANI YAIPA KENYA NDEGE ZA KISASA

Posted on Jul 21, 2012 | No Comments

Taarifa kutoka Marekani zinaeleza kuwa Wizara ya Ulinzi ya Marekani itaipatia Kenya ndege nane ndogo zisizohitaji rubani, ikiwa ni sehemu ya msaada wa kijeshi kwa nchi za Afrika Mashariki, ili kuzisaidia kupambana na wapiganaji wa Kiislamu wa Somalia, al-Shabaab.
Ndege isiyobeba rubani, drone
Gazeti la Wall Street Journal la Marekani limearifu kuwa Kenya itapata ndege hizo ambazo hazitakuwa na silaha, lakini zinaweza kugundua maeneo yanayofaa kulengwa na ndege au majeshi ya ardhini.
Gazeti hilo limesema ndege zisizokuwa na rubani ni sehemu ya msaada wa Marekani, pamoja na malori, zana za mawasiliano, na silaha kwa Burundi, Djibouti na Uganda.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru