BORIS BUNJAK KUTOKA SERBIA NDIYE KOCHA MKUU WA AZAM FC KWA MIAKA MIWILI
Posted on
Aug 7, 2012
|
No Comments

Boris Bunjak kocha mkuu mpya wa timu ya Azam FC akiipia picha wakati alipotambulishwa rasmi na uongozi wa timu hiyo leo jijini Dar es salaam, Boris Bunjak raia wa Serbia aliyezaliwa mwaka 1954 amesaini mkataba wa kuitukimia Azam FC kwa muda wa miaka miwili akiiitumikia timu hiyo, Boris Bunjak amefundisha timu mbalimbali katika nchi za kiarabu na amewahi kuchezaea timu ya taifa ya Serbia na vilabu mbalimbali huko Ulaya Mashariki amewahi kufanya kazi pia katika chama cha soka cha Yugoslavia mwaka 1993-1994 na kazi nyingine nyingi kuhusiana na masuala ya soka.
Mwenyekiti wa Azam FC mzee Said Mohamed Said akihijiwa na waandishi wa habari baada ya kumtangaza rasmi kocha wa timu yake ya Azam Fc ya jijini Dar es salaam, ambapo pia alisema kuhusu mchezaji Redondo ambaye anadaiwa kusajiliwa na timu ya Simba kwamba wao hwamzuii mchezaji huyo kwenda Simba isipokuwa Simba ifuate utaratibu wa Usajiri tu hawana tatizo na hilo