EBOLA YAIBUKA DRC PIYA
Posted on
Aug 19, 2012
|
No Comments
Ugonjwa wa Ebola umezuka kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Demokrasi ya Congo.
Wagonjwa wawili wamethibitishwa kuwa na virusi, mmoja wao amefariki.
Shirika la matibabu la MSF, lenye watu wake Isiro, linasema hatua zinachukuliwa ili kumtafuta na kumtenga mtu yeyote ambaye aliwakaribia wale walioambukizwa.
MSF inasema aina ya virusi vya Ebola ya Congo ni tofauti na ile ya Uganda, ambayo iliuwa watu 16 mwezi uliopita.