photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> > ETHIOPIA YAWA YA KWANZA AFRIKA KUNUNUA NDEGE AINA NA ‘BOEING 787 DREAMLINER’.

ETHIOPIA YAWA YA KWANZA AFRIKA KUNUNUA NDEGE AINA NA ‘BOEING 787 DREAMLINER’.

Posted on Aug 21, 2012 | 1 Comment

Shirika la Ndege la Ethiopia limekuwa la kwanza kumiliki ndege kubwa na ya kisasa kwa nchi za Afrika aina ya ‘Boeing 787 Dreamliner, na kuifanya kuwa nchi pekee Afrika kutumia ndege ya aina hiyo.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Ethiopian Airliner Tewolde Gebremariam amesema kwa kufikia uwezo huo inaonyesha jinsi gani Afrika inavyopiga hatua katika maendeleo duniani.
Ndege hiyo imewasili nchini Ethiopia kutoka uwanja wa ndege wa Dulles mjini Washngton, ambako kunaishi raia wengi wa Ethiopia.
Ndege hiyo mali ya Shirika la Ndege la Ethiopia linaloongoza kwa kukua kwa kasi, limenunua ndege hiyo kwa takriban dola milioni 207 za Marekani.
 

Comments:1