photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> > WIZARA YA FEDHA YAOMBA MKOPO BENKI YA MAENDELEO YA AFRIKA AfDB

WIZARA YA FEDHA YAOMBA MKOPO BENKI YA MAENDELEO YA AFRIKA AfDB

Posted on Aug 21, 2012 | No Comments

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Hussein Mwinyi.
WIZARA ya Fedha, imewasilisha ombi la Mkopo Benki ya Maendeleo Afrika
(AfDB) kwa niaba ya Jumuiya ya Afya ya Ukanda wa Mashariki, Kati na

Kusini mwa Afrika (ECSA-HC) ya kuwa na Kituo cha Afya kinachotarajiwa

kujengwa jijini Arusha.

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Hussein Mwinyi, alisema hayo

wakati akifungua mkutano wa sita wa Best Practices Forum and the 22

Directors’ Joint Consultative Meeting, uliofanyika jijini hapa.

Hayo yalisemwa jana na  Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya

Binadamu (NIMR) Dk. Mwele Malecela, ndiye aliyefungua mkutano huo kwa

niaba ya Waziri Dk. Mwinyi.
Alisema ujenzi wa kituo hicho umepangwa kujengwa eneo la Engare
Olmotonyi, nje kidogo ya jiji la Arusha, katika eneo la hekari 30

litakalotolewa na serikali.
“ Tanzania inafanyakazi na Jumuiya ya Afya ya ECSA ili
kuhakikisha utekelezaji wa ndoto ya muda mrefu ya kuanzisha kituo cha

afya cha kisasa cha kanda, ambacho kitakuwa na mambo mengi kama vile

Chuo cha Sayansi ya Afya ambacho kwa kiasi kikubwa kitaongeza nguvu

kuzalishwa watalaam,” alisema.

Aidha akizungumza na waanhishi wa habari kwa mahojiano zaidi  Dk.

Malecela alisema

 ni muhimu kwa nchi za Ukanda huo kubadilishana mawazo na uzoefu wa
namna wanazoshughulikia

suala la afya la uzazi na mtoto.
Alisema wajumbe watapata kuelewa namna nchi zingine zinavyotekeleza
suala la afya la mama na mtoto na kwa upande wa lishe bora.
Alisema mapendekezo ya mtakutano huo yatapelekwa kwa Baraza la
Mawaziri kwa utekelezaji na kuangalia namna ya kuongeza nguvu katika

upambana na magonjwa na suala muhimu ya raslimali watu katika sekta ya

afya.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru