KWA MSHANGAO WA WENGI BINTI WA WHITNEY HOUSTON ‘BOBBI KRISTINA BROWN’ AVISHWA PETE YA UCHUMBA NA KAKA YAKE WA KUFIKIA.
Posted on
Oct 12, 2012
|
No Comments
Mwezi
wa nane mwaka huu binti wa aliyekuwa mwanamuziki maarufu duniani
Whitney Houston anayekwenda kwa jina la Bobbi Kristina Brown alivishwa
pete na kaka yake wa kufikia Nick Gordon.
Pete hiyo
yenye kito cha madini ya ‘sapphire’ kilichozungukwa na chembe za almasi
iliyowekwa kidoleni kwa binti huyo, wadaku wameitafsiri kama alama ya
uchumba japokuwa wawili hao wamekana wakisema ilikuwa ni zawadi tu.
Hata
hivyo kipande cha kipindi cha mahojiano cha luninga alichorekodiwa binti
huyo mwenye umri wa miaka 19 kinachoitwa The Houstons: On Our Own
kidaiwa kuthibitisha kuwa binti huyo anachumbiwa na Gordon.
Nick
Gordon kijana mwenye miaka 22 amelelewa na hayati Whitney Houston kama
mwanae, hivyo ni sawa na kuwa kaka wa Bobbi Kristina Brown ambaye ghafla
baada ya kifo cha mwanamuziki huyo wameonyesha kupendana.