VURUNGU ZA WAISLAM MBAGALA KATIKA PICHA
Posted on
Oct 12, 2012
|
1 Comment
Vurugu
zilizofuatia mtoto anayeitwa Emanuel Josephat(14)’ kukojolea msaafu
(Quran) zimechukua sura mpya baada ya baadhi ya waumini wa dini ya
kiislam kukusanyika na kushinikiza mtoto huyo aachiwe na polisi ili
wamuue.
Waumini hao wanaokadiriwa kufikia idadi ya watu 3000 baada ya
kutawanywa na Polisi waliingia mitaani na kuchoma moto kanisa la
Kiinjili la Kilutheri Tanzania(KKKT), Mbagala Zakhem, wakaharibu Kanisa
la Anglican, wakavunja vioo vya kanisa la Wasabato, na kuchoma moto
Tanzania Assembly of God (TAG), la Mbagala Kizuiani na kuchukua vifaa
vya muziki vya kanisa hilo na kuvichoma moto hadharani.
Awali waumini hao walikusanyika katika kituo hicho cha polisi cha
Maturubai, Mbagala Kizuiani wakitaka mtoto huyo ambaye alikuwa chini ya
ulinzi wa polisi aachiwe na Polisi walipokataa matakwa yao ndipo vurugu
hizo zilipoanza.
Chanzo cha tukio hili ni mabishano baina ya watoto wawili, Emmanuel Josephat, na mtoto mwingine wa Kiislam.
Watoto hao walikuwa wakibishana kuhusu imani na dini ambapo mtoto wa
Kiislam alimwambia Emmanuel kuwa, “Quran ni kitabu kitakatifu, endapo
utafanya chochote kibaya juu yake basi utadhurika, waweza kuwa kichaa”.
Hapo ndipo Emmanuel alipoamua kuikojolea Quran ili kuona kama atakuwa kichaa.
Vurugu hizo ambazo zimesababisha gari za polisi namba T142 AVV,PT
0966 na T 325 BQP,basi la uda na gari la waandishi wa habari kutoka
Clouds zikiharibiwa kwa mawe na waandamanaji hao.
Kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) kilionekana kuzidiwa nguvu na watu
hao ambao walikuwa wakiwatawanya kutoka eneo moja wanakimbilia eneo
lingine na kuleta madhara mbalimbali ikiwa ni pamoja na kufunga
barabara.
Hatahivyo baada ya viongozi wa dini hiyo kufika wakiwa wameambatana
na Sheikh wa Wilaya ya Temeke, Sheikh wa Taasisi na Jumuiya za Waislamu
kukaa kikao na kamanda wa Polisi Wilaya ya Temeke, David Misime,
walifikia muafaka wa kuwaita waislamu hao na kuwatuliza lakini hali
iliendelea kuwa si shwari kwani baada ya viongozi hao kuona waandamanaji
hao wakikamatwa na kupigwa walikuja juu na kutishia kuondoka.
“Ndio nini sasa sisi tupo hapa kwa kuleta suluhu lakini ili waislamu
watulie lakini mnawapiga mbele yetu ndio nini sasa!?” alihoji mmoja wa
viongozi hao
Baadhi ya wafanya furugu wakipambana na polisi
Baadhi
ya vizuizi vilivyowekwa na waandamanaji katika eneo la Mbagala Kizuiani
katika harakati za kupinga kitabu kitakatifu cha Koran kukojolewa na
mtoto Emmanuel Josephat. Picha na Happy Mnale
Hamis Salum, baba wa mtoto ambaye Quran yake imekojolewa akiongea na vyombo vya habari
Mojawapo ya makanisa yanayosemekana kuharibiwa likiungua moto
FFU wakijiandaa kutuliza fujo
Mmoja ya wa waandamanaji akiwa amekamatwa na (FFU)
Moja ya gari lililoharibiwa katika vurugu hizo
Baadhi ya waandamanaji waliokamatwa wakipandishwa kwenye gari la polisi
Baadhi ya watuhumiwa wakiwa wamekamatwa na polisi
Polisi katika harakati za kuthibiti fujo
Baadhi ya watuhumiwa wakipandishwa kwenye gari la polisi
Polisi wakiwavusha baadhi ya watuhumiwa waliowakamata kwenye mfereji
Mmoja wa watuhumiwa akiwa amekamatwa na polisi
Moja ya magari la polisi yualiyoharibiwa
Sijui ni Mungu yupi ambaye hana nguvu na hata anapotendewa mabaya basi sisi tunakuwa na nguvu kuliko yeye kisha kulipizia Kisasi. Kama Taifa lazima tuondokane na ujinga huu. Dini inapotumika kuligawa Taifa na kulisambalatisha taifa hapo dini hiyo au watu wake wahusika hawapaswi kubaki kama walivyo.
ReplyDelete