WAZIRI MAGUFULI KUZINDUA JENGO LA TBA DODOMA JANA
Posted on
Oct 10, 2012
|
No Comments
Wizara
ya Ujenzi inapenda kuutarifu Umma kuwa leo Alhamisi ya tarehe
11/10/2012, Waziri wa Ujenzi atakuwa Mgeni Rasmi katika sherehe ya
kuweka jiwe la msingi katika jengo la ofisi linalojengwa na Wakala wa
Majengo Tanzania, Dodoma.
Sherehe za uwekaji jiwe la msingi zitafanyika eneo la Mpwapwa Flats, Mtaa wa Moshi kuanzia saa mbili asubuhi leo
Viongozi wa Serikali Mkoani Dodoma pamoja na Taasisi mbali mbali pia watashiriki katika sherehe hizo.
Mradi
huu wa jengo la ofisi ni mwendelezo wa azma ya Serikali kupitia Wakala
wa Majengo nchini wa kujenga majengo kwa ajili ya kupangishia shughuli
za ofisi.
Taarifa hii imetolewa na;-
Balozi Herbert Mrango
KATIBU MKUU.