photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> > NAULI ZA KWENDA MIKOANI ZAPANDA KINYEMELA

NAULI ZA KWENDA MIKOANI ZAPANDA KINYEMELA

Posted on Dec 8, 2012 | No Comments


Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni za mabasi wamepandisha nauli za mabasi kinyemela, licha ya Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (SUMATRA) kuwapiga marukufu. abiria mbalimabali wamekuwa wakitozwa kiwango cha juu tofauti na kile kilichowekwa na SUMATRA na kusababisha usumbufu kwa abiria. Uchunguzi ulifanywa na kugundua kuwa nauli kutoka Dar kwenda Mwanza imefikia kiasi cha sh 50,000/= badala ya sh 40,000/=, kwenda Iringa imepanda hadi sh 25,000/= badala ya sh 18,000/=, kwenda Masasi imefikia sh 25,000/= badala ya sh 22,000/=, Tunduma nauli kwa sasa ni sh 40,000/= badala ya sh 35,000/=. Imeelezwa kuwa wafanyakazi wa kampuni mbalimbali za mabasi wanakuwa na vitabu viwili vya kakatisha tiketi, abiria AKILALAMIKA KUWA NAULI KUBWA HUBADILISHA KITABU NA KUMKATIA TIKETI NYINGINE KWA BEI HALISI (ukiwabana wanakutoza nauli halisi) ila kama hujui viwango vya nauli hizi utatoa kiasi wanachotaka wao. Kwahiyo kuweni macho wadau mnaotumia usafiri huu muhimu wa mabasi yaendayo mikoani, hasa kipindi hiki cha mwisho wa mwaka. NAKUTAKIENI SIKUKUU NJEMA "X-MAS NA MWAKA MPYA".

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru