photo NAAZ_zpsd0bbd510copy_zps37715af5.jpg
 photo NAAZ_zpsd0bbd510.jpg
Nafasi Ya Matangazo
> > SERA YA NJE YA MAREKANI YAZIDI KUMTAFUNA OBAMA DHIDI YA MPINZANI WAKE ROMNEY.

SERA YA NJE YA MAREKANI YAZIDI KUMTAFUNA OBAMA DHIDI YA MPINZANI WAKE ROMNEY.

Posted on Oct 23, 2012 | No Comments

 Mitt Romney na Rais Barack Obama.
Rais Obama na mpinzani wake Mitt Romney wa   chama cha Republican wamepambana kwa hoja katika awamu ya  tatu na ya mwisho katika mji wa  Boca Raton-Florida, wakati zimebakia siku chache kufanyika uchaguzi.
Sehemu kubwa ya mdahalo wao wa muda wa saa moja na nusu ilikuwa juu ya sera ya nje ya Marekani  kuhusiana na Iraq, Afghanistan, Libya, Iran na Mashariki ya Kati.
Mgombea urais wa chama cha Republican Romney  amesema sera ya Obama ya kutumia nguvu dhidi ya wapiganaji wa kiislamu wenye  itikadi kali haitoshi katika kukomesha hatari ya siasa kali.
Romney amempongeza Rais Obama kwa kumzima  Osama Bin Laden na kwa kuwakabili viongozi wa al-Qaeda, lakini Romney ameeleza kuwa Marekani haiwezi kuondokana na hatari hiyo kwa njia ya kuua.
Amesema Marekani inapaswa kufanya zaidi ili kuwafanya watu katika nchi za kiislamu wapinge itikadi  kali.
 Akijibu hoja hiyo Rais Obama amesema mpinzani wake, Romney anafanya makosa katika kila suala  linalohusu sera ya nje.
Obama amesema ameifanya dunia iwe na usalama  zaidi tokea alipoanza kuwa Rais wa Marekani miaka minne iliyopita.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru